December 2, 2015

KIFO CHA ALEX MMOJA WA "GHETTO KIDS"




Irene Ngina                                                                                                              2/12/2015

 












Alex (katikati)
Picha kwa hisani ya wikipedia

 Mtoto alex ambaye ni mmoja wa watoto wanaounda kundi la “Ghetto kids” ambao wanafanya kazi na msanii toka uganda Eddy Kenzo, amefariki dunia huku mwingine kwa jina Patricia yuko hali mbaya baada ya kupata ajali ya baiskeli.
 Kwa mujibu wa William Mashal ambaye ni mmoja wa watu wao wa karibu sana amesema kwamba wawili hao walikuwa wakiendesha baiskeli ambayo ilikatika breki na kutumbukia mtaroni. Eddy Kenzo ametangaza kifo cha Alex jumatatu usiku huko Kampala Uganda.
Alex na Patricia walikuwa miongoni mwa “Ghetto kids” ambao walijipatia umaharufu duniani baada ya kucheza video ya wimbo wa Sityalos wa Eddy Kenzo na kuwa miongoni ya video zilizotazamwa ulimwenguni kote.

 https://soundcloud.com/eyereen-931981221/kifo-mp3

No comments: