November 16, 2015




 WAIGURU AHOJIWA NA EACC

Waziri wa Ugatuzi na Mipango ya Taifa Anne Waiguru yuko katika makao makuu ya Tume ya Maadili na Kukabili Ufisadi, EACC.Waiguru amewasili katika ofisi za EACC akiwa ameandamana na Wakili wake Ahmed Nassir Abdulahi. Kiongozi huyo anatarajiwa kuhojiwa  kuhusu madai ya ufisadi katika wizara yake pamoja na shutma za kutoajibikia ofisi yake,Kuhojiwa kwake kunajiri wakati mamia ya vijana waliobebea mabango kumsifu Waiguru wakiandamana nje ya ofisi ya EACC.Masaibu ya Waiguru yalianza mwezi Juni wakati uchunguzi ulipobaini kuwa shilingi milioni mia saba tisini na moja ziliporwa na sheria za ununuzi wa mali ya umma kukiukwa katika Taasisi ya Huduma kwa Vijana, NYS.

BY CRANE SENTEMAN.              

No comments: